Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Haya hapa majina ya waliochaguliwa kidato cha tano, vyuo

Wanafunzi 149,818 sawa na asilimia 69.96 wamechaguliwa kujiunga na masomo ya kidato cha tano, huku 64,323 wakichaguliwa kujiunga na vyuo vya elimu ya ufundi na ualimu.

Jumla ya wanafunzi 214,141 wakiwemo wasichana 97,517 na wavulana 116,624 ilibainishwa wana sifa za kuchaguliwa kujiunga na masomo ya kidato cha tano na vyuo vya elimu ya ufundi ikijumuisha wanafunzi 1,028 wenye mahitaji maalumu.



Waziri wa Nchi katika Ofisi ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Mohamed Mchengerwa ameyasema hayo leo Juni 6, 2025 wakati akizungumzia kuhusu uchaguzi wa wanafunzi wa kidato cha tano na vyuo mbalimbali.

Orodha ya wanafunzi waliochaguliwa na fomu za kujiunga na kidato cha tano, vyuo vya elimu ya ufundi mwaka, 2025 inapatikana katika tovuti ya Ofisi ya Rais -Tamisemi ya www.tamisemi.go.tz na Baraza la Taifa la Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi www.nactvet.go.tz.


OSZAR »