Rais wa Tanzania ambaye pia ni Mwenyekiti wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC-Organ), Samia Suluhu Hassan akishiriki mkutano wa dharura wa wakuu wa nchi na Serikali wa SADC kwa njia ya mtandao pamoja na viongozi mbalimbali, Ikulu Chamwino mkoani Dodoma leo Alhamisi Machi 13, 2025.
Mkutano huo pamoja na mambo mengine unajadili hali ya ulinzi na usalama Mashariki mwa nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC).